About Me

i am swalwhe kiluvia ,i would like to have defefernt frends to share idea

Sunday, November 6, 2011

NI lINI WANAHABARI MTAJIKOMBOA ?


Kuwepo kwa vyombo vingi vya habari hapa nchini Tanzania kuanzia miaka ya 80 kulipokelewa kwa mikono miwili na kuwepo kwa matumaini makubwa ya kupata malipo yaliyo bora lakini kinyume chake tumeshuhudia vyombo hivyo haviwanufaishi walengwa badala yake vinazidi kuwanyonya na kuwakandamiza na kudumaza taaluma na ufanisi .
Siku zote kumekuwepo na juhudi zinazofanywa na wanaharakati wanaotetea uhuru wa habari lakini hawajahi kutokea kutetea masilahi  na haki sitahili za mwanahabari ambae kukiwa na shida anaonekana ni muhimu  lakini tatizo linapokwisha hakumbukwi .
Cha kushangaza ni kuwa wanaharakati hao ambao tumekuwa tukiwashuhudia kushika mabango juu ya mambo  mbalimbali ya ukandamizaji yanapotokea katika taasisi au jamii fulani,wameshindwa kugeuza mabango hayo kuwateta wanahabari dhidi ya wamiliki wa vyombo hivyo ambao wanajiona ni sawa na miungu watu hawako tayari kutoa maslahi yaliyo bora kwa wanahabari.
kukosekana kwa chombo cha kutetea masilahi ya wanahabai kumesababisha kuwepo kwa rushwa  miongoni mwa wanahabari hasa wahariri ili kuweza kujikimu kimaisha hali ambayo ni hatari kwa utoaji wa habari za haki na ukweli ambazo haziegemei upande wowote wa jamii.
Ukiuliza wanahabari wanamtumikia nani jawabu lake ni moja tu ambalo ni rahisi sana watasema wanamtumikia  mwanasisa na mfanyabiashara kwa ajili ya masilahi ili kupata payola, na sio jamii kama wengi wanavyofikiri.

No comments:

Post a Comment