About Me

i am swalwhe kiluvia ,i would like to have defefernt frends to share idea

Sunday, November 6, 2011

DEMOKRASIA SIO VURUGU.

KUWEPO kwa vyama vingi vya siasa katika mataifa mbalimbali barani Afrika hasa yanayoendelea ni utamaduni mpaya ambao waafrika wameshindwa kuutumia kama ipasavyo na badala yake  mfumo huo unatumika kama sehemu ya vurugu na kulipiziana visasa na kukomoana.
 Tumekuwa tukishuhudia mara kwa mara kuwepo kwa mwingiliano au uvamizi wa chama kimoja kuvamia eneo ,mashina ya wakereketwa, wafurukutwa au maskani ,ambayo ni  ngome ya chama kingine kwa kisingizio cha kutafuta wafuasi na  kufungua matawi hapo jirani hii inaonysha wazi kuwa wahusika hawajakomaa kisiasa.
Mfano wa hivi karibuni ni chama kimoja chaupinzani kaskazini mwa Tanzania, kilivamia katika eneo la chama tawala na kung;oa mlingoti wa bendera ya chama tawala na kupora bendera kasha kubadilisha shina na kupandisha bendera ya chama hicho hali iliyopelekea wafuasi wanane wa chama hicho cha upinzani kukamatwa na polisi.
Jehiyo ndio demokrasia ya vyam vingi? Au huo ni uchanga wa kisiasa?je siasa za aina hii zinatrupeleka wapi,akili ya kuambiwa changanya na yako wahenga walisema.

No comments:

Post a Comment