About Me

i am swalwhe kiluvia ,i would like to have defefernt frends to share idea

Sunday, November 6, 2011

NI lINI WANAHABARI MTAJIKOMBOA ?


Kuwepo kwa vyombo vingi vya habari hapa nchini Tanzania kuanzia miaka ya 80 kulipokelewa kwa mikono miwili na kuwepo kwa matumaini makubwa ya kupata malipo yaliyo bora lakini kinyume chake tumeshuhudia vyombo hivyo haviwanufaishi walengwa badala yake vinazidi kuwanyonya na kuwakandamiza na kudumaza taaluma na ufanisi .
Siku zote kumekuwepo na juhudi zinazofanywa na wanaharakati wanaotetea uhuru wa habari lakini hawajahi kutokea kutetea masilahi  na haki sitahili za mwanahabari ambae kukiwa na shida anaonekana ni muhimu  lakini tatizo linapokwisha hakumbukwi .
Cha kushangaza ni kuwa wanaharakati hao ambao tumekuwa tukiwashuhudia kushika mabango juu ya mambo  mbalimbali ya ukandamizaji yanapotokea katika taasisi au jamii fulani,wameshindwa kugeuza mabango hayo kuwateta wanahabari dhidi ya wamiliki wa vyombo hivyo ambao wanajiona ni sawa na miungu watu hawako tayari kutoa maslahi yaliyo bora kwa wanahabari.
kukosekana kwa chombo cha kutetea masilahi ya wanahabai kumesababisha kuwepo kwa rushwa  miongoni mwa wanahabari hasa wahariri ili kuweza kujikimu kimaisha hali ambayo ni hatari kwa utoaji wa habari za haki na ukweli ambazo haziegemei upande wowote wa jamii.
Ukiuliza wanahabari wanamtumikia nani jawabu lake ni moja tu ambalo ni rahisi sana watasema wanamtumikia  mwanasisa na mfanyabiashara kwa ajili ya masilahi ili kupata payola, na sio jamii kama wengi wanavyofikiri.

DEMOKRASIA SIO VURUGU.

KUWEPO kwa vyama vingi vya siasa katika mataifa mbalimbali barani Afrika hasa yanayoendelea ni utamaduni mpaya ambao waafrika wameshindwa kuutumia kama ipasavyo na badala yake  mfumo huo unatumika kama sehemu ya vurugu na kulipiziana visasa na kukomoana.
 Tumekuwa tukishuhudia mara kwa mara kuwepo kwa mwingiliano au uvamizi wa chama kimoja kuvamia eneo ,mashina ya wakereketwa, wafurukutwa au maskani ,ambayo ni  ngome ya chama kingine kwa kisingizio cha kutafuta wafuasi na  kufungua matawi hapo jirani hii inaonysha wazi kuwa wahusika hawajakomaa kisiasa.
Mfano wa hivi karibuni ni chama kimoja chaupinzani kaskazini mwa Tanzania, kilivamia katika eneo la chama tawala na kung;oa mlingoti wa bendera ya chama tawala na kupora bendera kasha kubadilisha shina na kupandisha bendera ya chama hicho hali iliyopelekea wafuasi wanane wa chama hicho cha upinzani kukamatwa na polisi.
Jehiyo ndio demokrasia ya vyam vingi? Au huo ni uchanga wa kisiasa?je siasa za aina hii zinatrupeleka wapi,akili ya kuambiwa changanya na yako wahenga walisema.