About Me

i am swalwhe kiluvia ,i would like to have defefernt frends to share idea

Sunday, October 30, 2011

DEMOKRASIA NI JANGA AFRIKA

Demokrasia katika nchi za kiafriika inakuwa ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha sana, kwa kuwa inatumika kuleta machafuko na ghasia ambazo hupelekea  mamia na maelfu ya watu kupoteza maisha yao na pia kuharibu uchumi wanchi na watu , hususan kina mama na watoto hiutaabika sana.
Wengi wa wanasiasa  huwa na ubinafsi haramu, kwa kuwa hutumia damu za watu ili kujitafutia umaarufu na ushujaa ilihali wahanga wa wanasiasa hao husahalika maratu wanapozikwa, utwashangaa wanasiasa hao  baada ya mauaji ya raia wao hukaa meza moja na mahasimu wao wakipata shushu huku raia wakipotea muelekeo kwakuwa kutokana na fitna za wanasiasa huwasababishia kupoteza uchumi wao hata ule mgodo walio kuwa nao kwa nini hawakaa kabla ya kuleta madhara?
Ni vema wananchi kuwa macho na wanasiasa hawa uchwara ambao hutumia kigezo cha demokrasia kwa kupalilia vyeo vyao na vitambi vyao bila kujali maisha ya watu mali zao kwa kupandiza ugomvi na fitna ili  kugombanisha watu kwa manufaa yao binafsi.
Wanasiasa wengi wa waafrika huenda kinyume na falsafa wa Raisi wa zamani wa marekani aitwaye John Kennedy, kwa kifupi alifahamika kwa J.F.K alisema kabla ya kugombea uongozi ni vema kujiuliza utifanyia nini nchi yako badala ya kusema nchi yako itakufanyia nii, lakini lakushangaza na kustaajabisha ni kwamba vionozi wengi wa kiaafrika hutafuta madaraka kwa nguvu kwa minajili ya kujilimbikizia mali na kutafuta ukubwa bila kujali maisha au mali za watu kiasi gani zaweza kuteketea kwa kupitia choko choko zao , huku wao wenyewe hukimbilia nchi nyengine mambo yakiharibika.
Napenda kutoa mfano halisi ni tukio ambalo lilitokea ya hivi karibuni kaskazini mwa Tanzania  ambapo kiongozi mmoja wa kisiasa aliwashawishi wafuasi wake kwenda katika kituo cha polisi kutoa baadhi ya viongozi waliokuwa wakishikiliwa na jeshi hilo kwa ukkufanya maandamano bila kuwa na kibali, kauli ya mwanasiasa huyo ilikua kama ifuatavyo napenda kunukuu baadhi ya maneno ‘haya wote tuondoke hapa kwa pamoja twende tukawatoe viongozi wetu katika kituo cha polisi, kina mama na watoto waende nyumbani haya twendeni moja, mbili, tatu twende!!!’ lakini chakushangaza hapakuwepo na kiongoz hata i mmoja alieandamana na wafuasi hao. Kila mmoja alitafuta njia yake wengine walikimbilia mahotelini na wengine majumbani. Huku watu wengine wakipoteza maisha na wengine kujeruhiwa Je hi I ndo sawa?
Napenda kutumia fursa hii kuwashauri wananchi wezangu, akili za kuambiwa changanya na zako.