KUMBE UONGOZI CHADEMA NI MTIHANI MZITO ZITO
Mgogoro wauongozi ndani yachadema ulianza punde tu baada ya Zito Zuberi Kabwe kutangaza zamira yake yake ya kugombea nafasi ya uwenyekiti wa chama hicho jambao ambalo liliibua sintofahamu kati yake na mwenyekiti alioko madarakani Freeman Mbowe.
Sakata hili lililazimu baadhi ya wazee akiwemo inayesemekana kuwa mkwe wa Feeman Mbowe ambaye pia ni muasisiswa chama hicho Ediwini kutoa msimamo mkali kuamuru Zito kabwe atoa jina lake mara moja ,lakini hata hivyo Zito alikuwa ngangari nakutoamsimamowake kuwa asingetoa kwa kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia.
Lakini mambo yalizidi sana na kuona kumbe ndani ya chama chake hakuna demokrasiaaliamua kuachia ngazi ,ndipo walipomuahidi kumpa cheo cha ukatibu mkuu,lakini hata hivyo walimpa cheo cha naibu katibu mkuu.
Lakini mambo hayakuishia hapo baada ya uchaguzi wa Urais na Ubunge wa mwka huu 2010 kumalizika pia Zito alitangaza dhamira yake yakutaka kugombea kuwa kiongozi wa upinzani bungeni,lakini ilionesha dhahiri mwenyekiti wake Mbowe hakuridhika kumuunga mkono na nakumbidi kutoa kauli yakuwa mchakato wakupata kiongozi huyo utajadiliwa na chama.
Lakini tulichokiona baadae ni kuonaMbowe ndie alichaguliwa kuwa kiongozi wa upinzanibungeni na Zito Kabwe kuwa naibu wake,wachambuziwamambo husema kupata cheo hichopengine alitumia fedha zake katikakuwafadhili baadhi yawabunge wakati wa kampena hivyo walifanya hivyo kulipa fadhila.
Kitendo cha Zito kuomba kiti hicho pia wachambuzi hao wameelezea pengine imeongeza hasira za Mbowe hivyo kuenda mbali zaidi kutumia wabunge walealiowadhamini kuhakikisha wanamnyangaya hata nafasi ya unaibu katiaka kamba ya upinzani bungeni kupitia chadema nap engine kumfukuza uanachama.
Chama hakijaweka utaratibu wa namna kiongozi wa upinzani bungeni anapatikana. Utaratibu ukishawekwa nitatoa taarifa rasmi ila kwa sasa pitia Facebook yangu utaona ujumbe wangu,” alisema Zito
Mwenyekiti huyu wa chadema hakuanza mgogoro wa watu waonataka kugombea uongozi na Zito Peke yake, lakini pia alikugombana na alikuwa makamu mwenyekuti wa chama hicho Chacha Wange,Devid Kafulila na viongozi wengine ambao walijiondoa chadema na kudaikuwa chama hicho kinaongozwa na watu wawili kama kamuni yao.
Chacha wange yeye kizazaa kilibuka alipo hojii matumizi ya Ruzuku napia kutangaza nia yake ya kuta kugombea nafasi ya uwenyekiti katika chama hicho,hali ambayo ilisababisha mtafarukuhadi kifo chake ambacho kilizua utata alipo kuwa akirejea bungeani dodoma july 2008.
No comments:
Post a Comment